Friday, January 27, 2012

FANYA HAYA KWA MPENZI WAKO MTAISHI MUDA MREFU KWENYE MAHUSIANO.

Hakuna binadamu asiyefahamu nini maana ya mapenzi na kama wapo basi ni wachache sana na wanaweza kuwa hawafahamu kwa maneno lakini kivitendo wanakuwa wanafahamu aidha kwa kuona, kusikia na hata kwa wao wenyewe kushiriki kwenye mapenzi hayo.

Na hakuna binadamu yeyote asiyependa kupenda au kupendwa, wote tunapenda kupenda na pia tunapenda kupendwa in return. Na siku zote ukipenda na usipopendwa pale unapopenda huwa inakuwa ni huzuni sana na wengine hufikia hatua mbaya sana za kufikiria mengine mengi tu ya hatari pale mapenzi yanapokuwa machungu kwao.

Hii ndio sababu wengi wetu huwa tunakaa pale tunapoona kweli kuna mapenzi na si kukaa pale ambapo unaona unadanganywa au kuzungushwa kila siku. Lakini kuna wakati tunaweza kujikuta hata pale tunapopenda na kupendwa pia panaharibika baada ya muda na kunakuwa na ugomvi na kukosa maelewano baina yenu na wakati mwingine usifahamu kwa nini hamuelewani au ukaelewa lakini ukakosa njia za kutatua.

Zifuatazo ni baadhi tu ya njia mbalimbali za kufanya ukae na mpenzi wako kwa muda mrefu kwenye mahusiano na mkafurahia mapenzi yenu popote pale mtakapokuwa na mtakapoishi.

1. KUWA NA MUONEKANO CHANYA (POSITIVE IMAGE) KWA MPENZI WAKO.
Ukiwa Ni Mtu Wa Kuangalia Mabaya/Kasoro Sana Kwa Mpenzi Wako Kuliko Mazuri Yake Hautakuja Kukaa Kwenye Relationship Kwa Muda Mrefu Hata Siku Moja...Utaendelea Kubadilisha Wanaume/Wanawake Kila Siku Na Mwisho Wa Siku Utajiona Huna Bahati Kwenye Mapenzi Na Wakati Unayeyaharibu Mapenzi Yako Ni Wewe Mwenyewe...Hakuna Asiye Na Kasoro (Ukiwemo Wewe Mwenyewe). Kwa Hiyo Muonyeshe Mpenzi Wako Mapenzi Bora Na Umrekebishe Pale Anapokosea Bila Kuwa Na Lawama Mara Kwa Mara, Kuna Makosa Mengine Ni Madogo Sana Na Unaweza Kuyarekebisha Kwa Kukaa Chini Na Mpenzi Wako Mkayamaliza Kwa Dakika 5 Tu Lakini Wengine Huwa Issue Kubwa Kwao Na Kusababisha Mwisho Mbaya.

2. SAMEHE NA KUSAHAU.
Unapomsamehe mpenzi wako kwa kosa lolote alilokosa basi hakikisha umemsamehe kiukweli na ujitahidi kusahau kosa alilotenda itasaidia uwe na amani ya moyo zaidi kuliko kumsamehe kwa usoni tu lakini moyoni ukawa na Donge bado, hii hupelekea kupunguza mapenzi kwa kiasi Fulani kwake na kujikosesha furaha ya mapenzi.Anapokosea siku nyingine usimkumbushe kosa lake la nyuma kwa sababu itamfanya ajione mwenye huzuni na ajione kuwa hakusamehewa.

3. MPE NAFASI/UHURU MPENZI WAKO.
Mnapokuwa kwenye mahusiano jitahidini kwa hali na mali kupeana nafasi/uhuru kwenye mambo mengi hasa yale ya kitaaluma zaidi na kimaisha.anapokwambia yupo kwenye kikao cha kikazi jaribu kumuelewa na umpe support ya kutosha kwenye kazi zake au biashara zake au hata masomo yake.usipende sana kulalamika pale anapochelewa kurudi kazini au kutoka kwenye biashara zake bali mpokee kwa upole na baada ya kupumzika ndipo muulize kwa upole na kimahaba zaidi kwanini siku hizi anachelewa sana kurudi au kwenye biashara zake au shuleni tofauti na zamani.Hii itajenga zaidi kuliko kubomoa kwa kulalamika na kupayuka mbele yake na huku yeye akiwa hata hajapumzika na itamfanya siku nyingine aione nyumba chungu kitu ambacho si kizuri kwenu wote wawili.

4. KUWA MBUNIFU KWENYE MAPENZI.
Napozungumzia ubunifu hapa nakuwa simaanishi kwenye upande mmoja tu wa kwenye yale mambo yetu ya chumbani, hapana. Hapa namaanisha ubunifu kwenye mambo mengi ndani na nje ya nyumba, jitahidi mara kwa mara kubuni vitu vipya vitakavyofanya azidi kukupenda na kukuona kama mpya kwake kila siku. Kama amezoea kupata zawadi za aina Fulani kutoka kwako basi jitahidi siku moja kumbadilishia zawadi kutegemea na unavyomfahamu mpenzi wako anapenda nini na nini. Hakuna anayemjua mpenzi wako zaidi kuliko wewe kwa hiyo lazima ujue ukifanya nini kwake na kwa wakati gani atafurahia na kujivunia kuwa nawe.

5. WHAT GOES AROUND COMES AROUND.
Unapokuwa kwenye mapenzi hakikisha kwa khali yoyote humfanyi mpenzi wako awe na huzuni kila mara. Hapa ninamaanisha kuwa USIPENDE KUMFANYIA KITU UNACHOONA AKIKUFANYIA WEWE UTAKOSA FURAHA. Hakuna kitu kibaya kwenye mapenzi kama kukosa mapenzi uliyoyategemea kutoka kwa mpenzi wako. Kama unaona mpenzi wako aki-cheat utaumia sana basi hata yeye siku uki-cheat ataumia tena inawezekana kuliko wewe utakavyoumia. Usimfanyie kitu amabacho wewe hupendi kufanyiwa hata siku moja.

6. MFANYE AJIVUNIE KUWA NAWE.
Hakikisha katika mapenzi yenu kila siku unamfanya mpenzi wako ajivunie kuwa nawe na hakikisha humfanyi ajute kwa kukuchagua wewe miongoni mwa wote aliowaona. Usijidanganye hata siku moja kuwa kwa kumpata tu na kwa yeye kukupenda basi hajaona mwingine wa kuweza kuwa naye. Wapo wengi sana anaoweza kuwa nao lakini amekuchagua wewe katika hao wote, kwa hiyo usimfanye aanze kuwafikiria wale wengine wanaomfuatilia kila siku na kumsumbua.Ukianza kumwacha aanze kuwafikiria wengine aidha kwa wewe kuwa unamkosesha amani ya mapenzi kila mara au kwa mengine mabaya ndani ya mapenzi basi ipo siku utaishia pabaya.

7. MSAIDIE KWA KHALI NA MALI.
Kwenye mahusiano huwa kuna kupanda na kushuka miongoni mwa wapenzi na hasa kiuchumi na hata kisaikolojia. Hakuna kitu kizuri kwenye mapenzi kama mtu kupata tatizo na akasaidiwa na mpenzi wake katika hali ambayo hakuitegemea, namaanisha mpenzi wako akipata tatizo lolote hakikisha wewe ndo unakuwa wa kwanza kulifahamu na kulifanyia kazi. Sio matatizo yote yanamalizwa kwa pesa so hata ushauri na kumpa mawazo chanya inasaidia sana na kumfanya awe na furaha kuwa nawe.Kama unampenda usione tabu kumsaidia kwa kuogopa kuonekana eti unahonga, huyo ni mpenzi wako kwa hiyo jiamini na umpe kile anachostahili kusaidiwa na mpenzi wake.

Yapo mambo mengi sana ambayo kama mkiyafanya kwenye mapenzi basi uhusiano wenu utakuwa wa kudumu na wenye furaha sana ingawa hapa nimezungumzia kwa uchache sana lakini nina imani itasaidia sana kwa wote walio kwenye mahusiano .
Mapenzi hayana ndumba au limbwata hata siku moja, unapoona wapenzi wengi wana furaha kwenye mapenzi yao ni kwa sababu wanavumiliana kwa mengi na kusameheana kwa mengi.!!

Wednesday, January 25, 2012

JINSI YA KUONGEZA MAPENZI YALIO JUU KWA MPENZI WAKO

Hakika unahitaji akiwa mbali awe anatamani aone sura yako au asikilize sauti yako au hata asome SMS tamu iliyoandikwa kitaalamu na vidole vyako.

Hii ni hatua kubwa zaidi katika mapenzi. Ukiona mwenzi wako amefika kwenye kiwango hicho cha upendo, maana yake unamkonga kwelikweli. Amekushiba na umejaa ndani ya kuta za moyo wake.Hayo hayaji kama zawadi.

Mapenzi huzaliwa, hustawishwa kabla ya kukua. Kuna mambo ambayo unatakiwa uyafanye kuhakikisha mwenzi wako anakuza upendo wako kwako. Ni kama msemo wa ukiona vyaelea vimeundwa.Jinsi ya kumchombeza mtu, hutegemea pia jinsia.

Yapo mambo ambayo mwanamke anapenda aambiwe na mwenzi wake pia yapo matarajio ya wanaume kwa wapenzi wao.Kupitia yote hayo, tutayatazama katika muktadha mpana.


YAMPENDEZAYO MWANAMKE
Hapa chini kuna maneno 10 ambayo huwapendeza wanawake wengi. Yazingatie:

WEWE NI MREMBO (You’re beautiful)
Kiswanglish kinachukua nafasi pana hapa kwetu, kwa hiyo unaweza kumwambia kwa Kiswahili au Kiingereza, muhimu ni kuangalia jinsi anavyoweza kufurahia. Inawezekana akawa si mrembo kama Irene Uwoya au Jokate Mwegelo lakini unayo nafasi ya kumfanya ajione yupo sawa nao. Mwambie kuwa akivaa, hutoka bomba kuliko hao. Mtamkie maneno hayo asubuhi kabla hamjaachana kwenda kazini. Neno lako litamfanya ajiamini siku nzima.

UNAYAWEZA (You’re a great lover)
Kama wewe una bahati ya kupata mwenzi ambaye amepita unyagoni na kufuzwa kimitindo, ni heri yako.
Ikiwa uliyenaye hajiwezi, basi usisite kumwambia kwamba ukiwa naye faragha, anakutosheleza kwa asilimia 100. Unaweza kumchombeza kwa kumwambia afanye ziada ili kukufurahisha lakini tangulia kumsifia.

Wanawake wengi, hupenda kujua kama wanaume wao wanatosheka pindi wanapowapa huduma ya faragha.
Ukimsifia, unampa amani ya moyo na kumfanya ajiamini.

UNA AKILI SANA (You’re so smart)
Mwanamke hupenda kuonekana ana akili. Kama kuna kitu ambacho unaweza kumkwaza mwenzi wako ni pale utakapomtamkia kwamba yeye ni mjinga. Mfanye ajione ni bora kwa kumwambia kuwa ana akili sana. Mueleze kuwa kutokana na akili alizonazo, unaamini familia yenu itapata maendeleo makubwa kwa sababu ubongo wake ni hazina.


WEWE NI RAFIKI MKUBWA
(You’re my best friend)
Mwanamke wako anakupenda sana. Siyo tu kwamba anataka kuwa mpenzi wako bali pia anahitaji awe rafiki yako mkubwa. Mwambie kuwa huna rafiki mkubwa kama yeye chini ya jua.

Mchombeze kwamba huna mtu mwingine wa kuchangia naye siri zako zaidi yake. Hii inamaanisha kuwa mwanamke hapendi kuwa kimbilio lako la pili, daima hutaka kuwa wa kwanza ndani yako.


WEWE NI MUHIMU KWANGU 
(You’re the most important thing to me)
Inawezekana ukawa ‘bize’ mno na kazi. Unatumia muda wa wikiendi kuponda maisha na marafiki. Angalizo ni kuwa, usithubutu kumfanya mwanamke wako akahisi humuoni ni muhimu.

Pamoja na ‘ubize’ wako, tumia muda mchache unaoutumia na yeye kumuonesha jinsi alivyo muhimu. Isiishie hapo, mtamkie kwa herufi kubwa: “Wewe ni muhimu kwangu kuliko kitu kingine chochote duniani.”


SIKUDANGANYI
(I would never lie to you)
Mwanamke hujiamini pale anapobaini kuwa mwenzi wake ni mkweli. Anapokosea, hukiri na kuomba msamaha. Humchukia yule ambaye hujifanya kauzu, macho makavu anadanganya. Mwambie humdanganyi na umaanishe unachosema. Hayo yakijaa kwenye ubongo wake, utakuwa umempatia kwa kiwango kikubwa.

SIJAWAHI KUKUSALITI 
(I have never cheated on you)
Jaribu kuanzisha mazungumzo kuhusu namna ambavyo unachukia usaliti. Mbele ya mazungumzo yako, mueleze kuwa unaridhika kuwa naye, kwa hiyo hujawahi kumsaliti hata mara moja. Ni kawaida ya wivu kukua muda baada ya muda lakini wewe unayo nafasi ya kumfanya asiwe na chembe yoyote ya kukuhisi unamsaliti.

NINGEPOTEA BILA WEWE 
(I’d be lost without you)
Ni katika kumfanya ajione yeye ni taa ya maisha yako. Mueleze kuwa kama si yeye, ungeshapoteza muelekeo wa kimaisha. Kwa kawaida, mwanamke hataki tu kujua kuwa unampenda na kumtaka, ila unamhitaji kwa dhati, kwa hiyo ukimwambia ni yeye ndiye amekuweka kwenye mstari, atajiamini kuwa unamhitaji sana.

WEWE NI MCHESHI (You’re funny)
Daima tembea na kanuni hii. Wawili wanaopendana na kucheka pamoja ndiyo hudumu. Mpe uhuru akuchekeshe halafu uruhusu mbavu zako zivunjike kwa kicheko. Mwisho wa kicheko, gonganisha naye viganja halafu mwambie “wewe ni mcheshi sana mpenzi wangu.”

NAKUPENDA (I love you)
Ni neno la kawaida lakini kwa mwanamke huwa lina maana kubwa endapo litatamkwa na mtu anayempenda.

Upendo wa kweri ndio upi?

Upendo wa kweri sio tu maneno mazuri, na wala sio tu upendo wa matendo au wa kuleta maua na chokleti.
 
Bali ni kuonyeshana heshima uaminifu na imani. Kuonyesha wepesi wa kuona huruma wakati mwanzako anapokuwa na msongo/matatizo. Kuwa msaidizi mwema na mwenye kusema ukweli. na kuweza kuonyesha masikitiko yako kwa mwenzio.

Sio kila wakati kujifanya mwenye nguvu (mvumilivu)/ mjuaji wa kilakitu, bali  mkae/kaeni pamoja, mtatue issues pamoja, msaidiane pale mwenzako ameshindwa.
 
Usiwe wewe bali Kuweni ninyi kwa kila kitu mfanyacho. Muwe kila wakati mna furaha . Kama mmoja wenu ana uzuni basi uzunikeni pamoja.
 
Mshirikiane katika raha na shida, taabu na njaa kwenye maisha yenu.

Tuesday, January 24, 2012

THE WORD RELATIONSHIPS

Relationships move beyond friendship. They occur when two people feel emotionally attached, fulfill each other needs and generally feel interdependent. When a true relationship exists, several components are present:

Trust; relationships must be built on a foundation of trust. We need to be to count on others and feel that they will be open with us.
Honesty; no relationship can survive if the partner are no honest with one another. Each partner must share a commitment of truth. Those in good relationships accept one another, blemishes and all. A relationship based on untruth or even half-truth lacks depth and meaning.

Mutual support;
Healthy relationships are characterized by mutual support. A partner’s well-being should have an impact on you, and your well-being should affect your partner. In best way the partner seek out what is best for both, and they act as advocates for and defend each other.

Loyalty;
The mark of a good relationship is loyalty. Loyalty implies the relationship, partners are supportive of each other no matter what even in times of adversity and difficulty.

Acceptance;
Your best friend develops a love for the Dave Mathews band and listens to their CDs seemingly without interruption. You can’t stand to listen to them. Do you decide that you can no longer be friends to that person? Of course not.That is the same as for your partner, there things some time u can't stand it but if you love your man/woman then you gonna have to accept things as it is/ as it comes.